Ijumaa, 28 Agosti 2026

MTENDAJI MKUU ATEMBELEA KITUO CHA USULUHISHI, MAHAKAMA YA ARDHI

Na MWANDISHI WETU-Mahakama, Dar es Salaam

Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Dkt. John Jingu, tarehe 26 Agosti, 2026 alifanya ziara katika Mahakama Kuu ya Tanzania Kituo cha Usuluhishi pamoja na Mahakama Kuu Divisheni ya Ardhi kwa lengo la kujitambulisha.

Ziara hiyo imekuwa ya kwanza kufanyika tangu ateuliwe na kuapishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kushika wadhifa huo.

Lengo lingine lilikuwa kufahamu kwa kina utekelezaji wa majukumu ya Mahakama hizo, kutathmini mafanikio yaliyopatikana pamoja na kubaini changamoto zilizopo katika utekelezaji wa majukumu.

Akizungumza na watumishi, Dkt. Jingu aliwasisitiza kuwa na upendo, mshikamano na kufanya kazi kwa ushirikiano ili kuhakikisha Mahakama inaendelea kutoa huduma bora na kwa ufanisi kwa wananchi.

Alisisitiza umuhimu wa watumishi kushirikiana katika kutatua changamoto na kutekeleza majukumu yao kwa weledi, uadilifu na kujituma.

Katika ziara hiyo, Mtendaji Mkuu aliambatana na Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. Eva Nkya, ambaye aliwapongeza watumishi kwa kazi nzuri wanayoifanyika na kusisitiza umuhimu wa kutenga muda kwa ajili ya kufanya mazoezi ya mwili ili kuimarisha afya na ustawi wao wanapotekeleza majukumu yao kwa ufanisi.

Mhe. Nkya pia aliwahimiza watumishi wa Mahakama hizo kuiishi salamu ya Mahakama inayosisitiza uadilifu, weledi na uwajibukaji katika kazi na kuwataka kuwa na maadili na matumizi ya lugha nzuri wanapowahudumia wananchi.

Naye Kaimu Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kituo cha Usuluhishi, Mhe. Isaya Arufani, alimshukuru Mtendaji Mkuu kwa kufanya ziara hiyo, kufanya majadiliano na watumishi na kuahidi kuzifanyia kazi changamoto zilizowasilishwa.

Ziara hiyo imekuwa muhimu katika kuimarisha mawasiliano, ushirikiano na uongozi kati ya watumishi na uongozi wa Mahakama ya Tanzania, pamoja na kuweka msisitizo katika utoaji wa huduma bora na ufanisi wa Mahakama.

Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Dkt, John Jingu, akisalimiana na Kaimu Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kituo cha Usuluhishi, Mhe. Isaya Arufani. Kulia akishuhudia ni Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. Eva Nkya.

Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. Eva Nkya, akichukua nafasi yake baada ya kuwasili kwenye Ofisi za Mahakama Kuu Kituo cha Usuluhishi. Kulia ni Mtendaji wa Mahakama Kuu Kituo cha Usuluhishi, Bi. Hellen Mkumbwa.

Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Dkt. John Jingu (kulia) na Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. Eva Nkya (kushoto) wakizungumza na Kaimu Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kituo cha Usuluhishi, Mhe. Isaya Arufani (katikati).

Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Dkt. John Jingu, akisaini kwenye kitabu cha wageni katika Ofisi ya Mahakama Kuu Kituo cha Usuluhishi.

Mtendaji wa Mahakama Kuu Kituo cha Usuluhishi, Bi. Hellen Mkumbwa, akitoa utambulisho wa Viongozi mbalimbali kwa Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Dkt. John Jingu (hayupo kwenye picha). 


Viongozi wa Mahakama wakimsikiliza Kaimu Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kituo cha Usuluhishi, Mhe. Isaya Arufani (hayupo kwenye picha).

Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Dkt. John Jingu akiwa katika Ofisi ya Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Divisheni ya Ardhi, Mhe. Elinaza Luvanda (picha chini).



Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. Eva Nkya, akizungumza akiwa katika Ofisi ya Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Divisheni ya Ardhi.

Mtendaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Divisheni ya Ardhi, Bw. Donald Makawia, akitoa utambulisho wakati wa kikao hicho.

Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. Eva Nkya, akizungumza wakati wa kikao hicho. Katikati ni Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Dkt. John Njingu na kulia ni Naibu Msajili wa Mahakama Kuu Divisheni ya Ardhi, Mhe. Niku Mwakatobe (kulia) akichukua kumbukumbu muhimu wakati wa kikao hicho.


Sehemu ya watumishi wa Mahakama ya Tanzania, Kituo cha Usuluhishi na Divisheni ya Ardhi (juu na chini), wakimsiliza Mtendaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Dkt. John Njingu (hayupo katika picha).

Habari hii imehaririwa na FAUSTINE KAPAMA-Mahakama, Dodoma. 

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni