Na MUKSINI NAKUVAMBA - Mahakama, Mbeya
Watumishi
wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo ya Mbeya wamefanya ziara ya kikazi ya
kuzuru Makao Makuu ya Mahakama na Tume ya Utumishi wa Mahakama jijini Dodoma, kwa
lengo la kuongeza uelewa wa masuala ya kiutumishi, kujifunza mifumo ya
uendeshaji wa shughuli Mahakama na kubadilishana uzoefu ili kuimarisha utendaji
kazi na utoaji wa huduma.
Ziara
hiyo imeongozwa na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo ya
Mbeya, Mhe. Fahamu Mtulya, akiambatana na Viongozi pamoja na watumishi.
Aidha, Watumishi
hao walipata fursa ya kujifunza kwa kina kuhusu masuala yanayohusu utumishi
ndani ya Mahakama, ikiwemo utekelezaji wa majukumu kwa kuzingatia sheria,
kanuni, taratibu na miongozo inayosimamia utendaji wa Mahakama.
Aidha,
watumishi hao walitembelea Ofisi za Tume ya Utumishi wa Mahakama, ambako
walipata maelezo kuhusu majukumu ya Tume, hususan katika usimamizi wa masuala
ya rasilimali watu, nidhamu, maadili na maendeleo ya watumishi wa Mahakama.
Akizungumza
wakati wa ziara hiyo, Naibu Katibu Tume ya Utumishi wa Mahakama
anayeshughulikia Nidhamu na Maadili, Bi. Alesia Mbuya, aliwakaribisha watumishi
hao na kuwapongeza kwa kutenga muda wa kutembelea Ofisi za Tume, akieleza kuwa,
ziara hizo ni muhimu katika kuongeza uelewa na kuimarisha ushirikiano pamoja na
kubadilishana uzoefu katika masuala ya kiutumishi.
Kwa
upande wake, Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Masjala Ndogo ya Mbeya,
Mhe. Fahamu Mtulya, alieleza umuhimu wa watumishi kupata fursa za kujifunza
kutoka katika maeneo mbalimbali ya Mahakama, akisisitiza kuwa maarifa na uzoefu
unaopatikana kupitia ziara hizo ni muhimu katika kuboresha utendaji kazi wa
kila siku.
Mbali
na Ofisi za Tume ya Utumishi wa Mahakama, watumishi hao walitembelea maeneo
mbalimbali ya kimkakati katika Jengo la Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania,
ambako walijifunza namna matumizi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano
(TEHAMA) inavyotumika katika kurahisisha na kuimarisha utekelezaji wa majukumu
ya Mahakama.
Miongoni
mwa maeneo yaliyotembelewa ni ukumbi mpya wa mikutano ulioandaliwa kwa mifumo
ya kisasa ya TEHAMA, ambapo watumishi hao walijionea namna teknolojia
inavyowezesha uendeshaji wa mikutano, mafunzo na shughuli mbalimbali za
kitaasisi kwa ufanisi.
Vilevile,
walitembelea Chumba cha Mifumo ya TEHAMA, ambacho ni miongoni mwa maeneo muhimu
katika miundombinu ya kiteknolojia iliyopo ndani ya Jengo la Makao Makuu ya
Mahakama. Katika eneo hilo, watumishi walipata maelezo kuhusu uratibu,
usimamizi na uendeshaji wa mifumo ya TEHAMA inayosaidia shughuli za Mahakama.
Ziara
hiyo pia iliwapa watumishi hao fursa ya kutembelea Mahakama Kuu ya Tanzania
Masjala Ndogo ya Dodoma, ambako walipokelewa na na Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu
Masjala Ndogo ya Dodoma, Mhe. Joachim Tiganga.
Mhe.
Tiganga, aliwashukuru watumishi hao kwa dhamira yao ya kuendelea kuimarisha ushirikiano,
kujenga molari ya utendaji kazi kwa watumishi, matumizi ya teknolojia,
uwajibikaji na utoaji wa huduma bora kwa wananchi, kwa kuweka mkazo katika kujifunza,
kubadilishana uzoefu na kuendeleza rasilimaliwatu kama msingi wa ufanisi.
Viongozi
na Watumishi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya wakiwa Mbele ya jengo la
Tume ya Utumishi wa Mahakama walipotembelea katika ziara hiyo.
Viongozi
na Watumishi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya wakiwa kwenye picha ya pamoja
na mwenyeji wao Jaji Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Dodoma Mhe, Joachim
Tiganga, Mbele ya jengo la Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Dodoma walipotembelea
katika ziara hiyo.
Jaji
Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Fahamu Mtulya (katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja viongozi wa Masjala hiyo walipotembelea Mahakama Kuu Masjala Ndogo wa Dodoma.
Jaji
Mfawidhi Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya Mhe. Fahamu Mtulya (aliyesimama
mbele) akizungumza na watumishi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya walipotembelea
ofisi ya Tume ya utumishi wa Mahakama
Viongozi
na Watumishi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya wakiwa ndani ya ukumbi mpya
wakisasa uliopo ndani ya Jengo la Makao Makuu ya Mahakama.
Viongozi
na Watumishi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Mbeya wakiwa Mbele ya jengo la
Makao Makuu ya Mahakama jijini Dodoma.
(Habari Hii Imehaririwa na Innocent Kansha - Mahakama)

.jpeg)




.jpeg)
.jpeg)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni