Na ARAPHA RUSHEKE -Mahakama Kuu Dodoma.
Uongozi
wa Chama cha Wanasheria Tanganyika, Dodoma
Chapter, ukiongozwa Bi. Mary Munissi,
tarehe 21 Agosti,2026 umemtembelea Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo
Dodoma, Mhe. Joachim Tiganga,
katika ofisi yake iliyopo Kituo
Jumuishi cha Utoaji Haki (IJC) Dodoma.
Katika
kikao hicho, pande hizo zimezungumzia mambo mbalimbali ikiwemo changamoto
zinazowakabili, pamoja na namna bora ya kuimarisha ushirikiano kati ya Mahakama
na Wanasheria ili kuhakikisha huduma za utoaji haki kwa wananchi zinaendelea
kutolewa kwa ufanisi na kwa wakati.
Kikao hicho pia kimekuwa sehemu ya kuimarisha uhusiano na ushirikiano wa kitaaluma kwa lengo la kuboresha zaidi huduma za haki katika eneo la Dodoma.
Jaji
Mfawidhi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo Dodoma, Mhe. Joachim Tiganga, akisalimiana
na wageni kutoka TLS Dodoma mara baada ya kuwasili katika ofisi yake kwa
mazungumzo.
Naibu
Msajili wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo Dodoma, Mhe Upendo Ngitiri (aliyesimama)
akitoa neno la ukaribisho mara baada ya kuwasili kwa wageni hao.
Mwenyekiti
wa TLS Dodoma, Bi Mary Munissi (wa kwanza kushoto) akimsikiliza kwa umakini kilichokuwa
kinajiri.
Jaji
Mfawidhi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo Dodoma, Mhe. Joachim Tiganga (aliyepo
katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Mwenyekiti wa TLS Dodoma, Bi. Mary
Munissi (aliyepo kulia kwake) na aliyepo kushoto kwake ni Makamu Mwenyekiti wa
TLS Dodoma, Bw, Anselm Mwampoma.
Jaji
Mfawidhi wa Mahakama Kuu Masjala Ndogo
Dodoma, Mhe Joachim Tiganga (wa nne kutoka kushoto) akiwa katika picha ya
pamoja na sehemu ya uongozi wa TLS Dodoma mara baada ya kumtembelea ofisini
kwake.
Habari hii imehaririwa na FAUSTINE KAPAMA-Mahakama, Dodoma.





Hakuna maoni:
Chapisha Maoni