Alhamisi, 22 Januari 2026

JAJI MKUU, WADAU WAKUTANA NA KUJADILIANA UBORESHAJI HUDUMA ZA MAHAKAMA

Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. George Masaju leo tarehe 22 Januari, 2026   amekutana na kufanya mazungumzo na Wadau wa Mahakama lengo likiwa ni kujadiliana juu ya uboreshaji wa utoaji wa huduma za Mahakama na Sekta ya Sheria kwa ujumla.

Wadau walioshiriki katika kikao hicho ni pamoja na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Mhe. Hamza Johari, Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria, Mhe. Eliakim Maswi, Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Antony Sanga, Naibu Wakili Mkuu wa Serikali, Bi. Alice Mtulo, Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka, Bi. Bibiana Kileo na Wadau wengine. 

Kikao hicho kimefanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Jaji Mkuu Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania jijini Dodoma

Kwa upande wa Mahakama kikao hicho kimehudhuriwa na Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Mustapher Mohamed Siyani, Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. Eva Kiaki Nkya, Msajili wa Mahakama ya Rufani Tanzania, Mhe. George Herbert, Mkurugenzi wa Usimamizi wa Mashauri, Mhe. Desdery Kamugisha, Mkurugenzi wa Maktaba, Mhe. Kifungu Kariho na Maafisa wengine wa Mahakama.

Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania na Mwenyekiti wa Kikao, Mhe. George Masaju (aliyeketi mbele) akiongoza kikao cha pamoja na Wadau wa Mahakama waliohudhuria katika kikao hicho kilichofanyika leo tarehe 22 Januari, 2026 kwenye ukumbi wa mikutano wa Jaji Mkuu uliopo Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania jijini Dodoma.

Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. George Masaju akizungumza jambo wakati akifungua kikao cha pamoja na Wadau wa Mahakama kilichofanyika leo tarehe 22 Januari, 2026 kwenye ukumbi wa mikutano wa Jaji Mkuu uliopo Makao Makuu ya Mahakama jijini Dodoma.


Wadau mbalimbali pamoja na baadhi ya Viongozi na Maafisa wa Mahakama walioshiriki katika kikao hicho wakifuatilia kinachojiri katika kikao hicho.

Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Mhe. Hamza Johari akichangia jambo wakati wa kikao kati ya Jaji Mkuu na Wadau wa Mahakama kilichofanyika leo tarehe 22 Januari, 2026 kwenye ukumbi wa mikutano wa Jaji Mkuu uliopo Makao Makuu ya Mahakama jijini Dodoma.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria, Mhe. Eliakim Maswi akichangia jambo 
wakati wa kikao kati ya Jaji Mkuu na Wadau wa Mahakama kilichofanyika leo tarehe 22 Januari, 2026 kwenye ukumbi wa mikutano wa Jaji Mkuu Makao Makuu ya Mahakama jijini Dodoma.

Mkurugenzi wa Usimamizi wa Mashauri-Mahakama ya Tanzania, Mhe. Desdery Kamugisha akiwasilisha mada wakati wa kikao kati ya Jaji Mkuu na Wadau wa Mahakama kilichofanyika leo tarehe 22 Januari, 2026 kwenye ukumbi wa mikutano wa Jaji Mkuu Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania jijini Dodoma.


Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka, Bi. Bibiana Kileo akizungumza jambo wakati wa kikao kati ya Jaji Mkuu na Wadau wa Mahakama kilichofanyika leo tarehe 22 Januari, 2026 kwenye ukumbi wa mikutano wa Jaji Mkuu Makao Makuu ya Mahakama jijini Dodoma.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Antony Sanga akichangia jambo wakati wa kikao kati ya Jaji Mkuu na Wadau wa Mahakama kilichofanyika leo tarehe 22 Januari, 2026 kwenye ukumbi wa mikutano wa Jaji Mkuu Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania jijini Dodoma.

Naibu Wakili Mkuu wa Serikali, Bi. Alice Mtulo (kushoto) akizungumza jambo 
wakati wa kikao kati ya Jaji Mkuu na Wadau wa Mahakama kilichofanyika leo tarehe 22 Januari, 2026 kwenye ukumbi wa mikutano wa Jaji Mkuu Makao Makuu ya Mahakama jijini Dodoma. Kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. Antony Sanga.

Mdau kutoka Wizara ya Katiba na Sheria akichangia jambo wakati wa kikao hicho.

(Picha na MARY GWERA, Mahakama-Dodoma)











MSAJILI MKUU AFUNGUA MAFUNZO KWA MAAFISA MIREJESHO KITUO CHA HUDUMA KWA MTEJA

Na. HABIBA MBARUKU & JAMES BUSANYA, Mahakama-Dodoma

Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania Mhe. Eva Nkya leo tarehe 22 Januari, 2026 amefungua mafunzo kwa Maafisa Mirejesho wa Kituo cha Huduma kwa Mteja katika Ukumbi wa Chumba Maalumu cha Mifumo ya Utoaji Taarifa (Judiciary Situation Room) kilichopo Makao Makuu ya Mahakama jijini Dodoma.

Akizungumza wakati wa kufungua mafunzo hayo Mhe. Nkya amesema kuwa lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo watumishi wote wanaotekeleza majukumu yao katika Kituo cha Huduma kwa Mteja cha Mahakama ya Tanzania (Judiciary Customer Service Center zamani Judiciary Call Centre) katika matumizi ya mfumo ulioboreshwa wa mawasiliano na mteja, mfumo ambao ulianza kutumika katika toleo la kwanza ambao sasa umeboreshwa kwa kiwango kikubwa hadi kufikia toleo la nne.

Mhe. Nkya ameongeza kuwa maboresho hayo yametokana na uzoefu wa matumizi ya mfumo wa awali pamoja na tathmini ya mahitaji ya kiutendaji ili kuongeza ufanisi na kurahisisha upatikanaji wa huduma ya mawasiliano kwa wakati.

Maboresho haya yametokana na uzoefu wa matumizi ya mfumo wa awali pamoja na tathmini ya kina ya mahitaji ya kiutendaji kwa lengo la kuongeza ufanisi, ubora wa huduma na kurahisisha mawasiliano kati ya Mahakama na wananchi, amesema Mhe. Nkya

Aidha, Msajili Mkuu ameeleza kuwa, mfumo wa toleo la nne umeongezewa huduma mbalimbali ikiwemo kuunganishwa na WhatsApp Chatbot, hatua inayolenga kuisogeza Mahakama karibu zaidi na wananchi kwa kuwafikia kupitia majukwaa wanayotumia kwa wingi katika maisha ya kila siku.

Ameeleza kuwa tofauti na awali, mfumo huo sasa unaweza kutumika popote bila kuathiri utoaji wa huduma, hali itakayosaidia kuongeza ufanisi wa kazi na mwendelezo wa huduma kwa wananchi wakati wote.

Mhe. Nkya ameongeza kuwa, Maboresho mengine ni pamoja na uwezo wa watoa huduma kuwarudia wateja kwa kuwapigia simu moja kwa moja, kufanya ufuatiliaji wa masuala katika Mahakama yoyote nchini, pamoja na kuwa rafiki zaidi kwa mtumiaji kwa kupunguza makosa ya kibinadamu.

Vilevile, Mahakama imeimarisha upatikanaji wa huduma muda wote kwa kuanzisha Kituo cha Akiba cha Mfumo katika Mkoa wa Dar es Salaam, ili kuhakikisha huduma hazikatiki hata kunapojitokeza changamoto za kiufundi.

Sambamba na hayo Mhe. Nkya amesisitiza kuwa, baada ya mafunzo hayo, Mahakama inatarajia kuona ongezeko la ufanisi katika kushughulikia mawasiliano ya wananchi, matumizi sahihi ya takwimu katika kufanya maamuzi ya kiuendeshaji, pamoja na kuimarika kwa uwajibikaji na uwazi kwa watumishi.

Msajili Mkuu, ametoa wito kwa washiriki wa mafunzo hayo kutumia maarifa watakayoyapata kuboresha huduma, kuimarisha maadili ya kazi na kuendelea kujenga imani ya wananchi kwa Mahakama.

Masajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania Mhe. Eva Nkya akizungumza wakati alipokuwa akifungua mafunzo kwa Maafisa Mirejesho wa Kituo cha Huduma kwa Mteja, leo 22 Januari, 2026 katika Ukumbi wa Chumba Maalumu cha Mifumo ya Utoaji Taarifa (Judiciary Situation Room) kilichopo Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania  jijini Dodoma.

Naibu Msajili na Mkurugenzi wa Divisheni ya Ukaguzi wa Huduma za Kimahakama, Mirejesho kwa Umma na Maadili, Mhe. Maira Kasonde akitoa neno la utangulizi kabla ya kumkaribisha Msajili Mkuu wa Mahakama ili kufungua mafunzo kwa Maafisa Mirejesho wa Kituo cha Huduma kwa Mteja, leo 22, Januari, 2026 katika Chumba Maalumu cha Mifumo ya Utoaji Taarifa (Judiciary Situation Room) kilichopo Makao Makuu ya Mahakama jijini Dodoma.


Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania Mhe. Eva Nkya (wa pili kulia) akiwa katika picha ya pamoja na sehemu ya Maafisa Mirejesho wa Kituo cha Huduma kwa Mteja baada ya kufungua mafunzo kwa maafisa hao, katika Chumba Maalumu cha Mifumo ya Utoaji Taarifa (Judiciary Situation Room) Makao Makuu ya Mahakama jijini Dodoma, wengine ni Naibu Msajili na Mkurugenzi wa Divisheni ya Ukaguzi wa Huduma za Kimahakama, Mirejesho kwa umma na Maadili, Mhe. Maira Kasonde wa kwanza kulia.

Sehemu nyingine ya maafisa mirejesho wa kituo cha huduma kwa mteja wakiwa katika picha ya pamoja na Msajili Mkuu wa Mahakama Mhe. Eva Nkya (wa kwanza kushoto) baada ya kufungua mafunzo kwa maafisa hayo katika Chumba Maalumu cha Mifumo ya Utoaji Taarifa (Judiciary Situation Room) Makao Makuu ya Mahakama jijini Dodoma, (wa pili kushoto) ni Naibu Msajili na Mkurugenzi wa Divisheni ya Ukaguzi wa Huduma za Kimahakama, Mirejesho kwa umma na Maadili, Mhe. Maira Kasonde.


Sehemu ya maafisa Mirejesho wa Kituo cha Huduma kwa Mteja wakifuatilia hotuba ya Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania Mhe. Eva Nkya.

Sehemu ya maafisa Mirejesho wa Kituo cha Huduma kwa Mteja wakifuatilia hotuba ya Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania Mhe. Eva Nkya.

Maafisa Mirejesho wa Kituo cha Huduma kwa Mteja wakisikiliza hotuba ya Msajili Mkuu wa Mahakama Mhe. Eva Nkya (aliyesimama mbele) wakati wa ufunguzi wa mafunzo kwa Maafisa Mirejesho wa Kituo cha Huduma kwa Mteja, leo 22 Januari, 2026 katika Chumba Maalumu cha Mifumo ya Utoaji Taarifa (Judiciary Situation Room) kilichopo Makao Makuu ya Mahakama jijini Dodoma.

Sehemu ya Maafisa Mirejesho wa Kituo cha Huduma kwa Mteja wakifuatilia hotuba ya Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania Mhe. Eva Nkya (aliyesimama mbele)

(Habari Hii Imehaririwa na Innocent Kansha-Mahakama)


 

Jumatano, 21 Januari 2026

JAJI MKUU AFANYA MAZUNGUMZO NA BODI YA UDHAMINI WA TAARIFA ZA JUZUU LA SHERIA

Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. George Masaju leo tarehe 21 Januari, 2026   ametembelea na kufanya mazungumzo na Bodi ya Udhamini wa Taarifa za Juzuu la Sheria Tanzania (TLR) inayoendelea na kikao kazi chake kwenye ukumbi wa Maktaba Makao Makuu ya Mahakama Jijini Dodoma.

Kikao kazi hicho ambacho kilianza tarehe 19 Januari, 2026 kinalenga kuchambua maamuzi ya mwaka 2025 ya Mahakama ya Rufani, Mahakama Kuu ya  Tanzania na Mahkama Kuu ya Zanzibar kwa ajili ya kitabu cha Mwaka 2025.

Kikao kazi hicho kinatarajiwa kuhitimishwa tarehe 23 Januari, 2026.

Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. George Masaju akisaini kitabu cha wageni leo tarehe 21 Januari, 2026 alipoitembelea Bodi ya Udhamini wa Taarifa za Juzuu la Sheria Tanzania (TLR)  na kufanya mazungumzo na Bodi hiyo inayoendelea na kikao kazi chake kwenye Maktaba ya Makao Makuu ya Mahakama jijini Dodoma.

Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Mustapher Mohamed Siyani akisaini kitabu cha wageni alipotembelea Maktaba ya Mahakama katika kikao kazi cha Bodi ya Udhamini wa Taarifa za Juzuu la Sheria Tanzania (TLR) kinachoendelea kufanyika kwenye ukumbi wa Maktaba ya Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania jijini Dodoma. Aliyeketi mbele ni Katibu wa Bodi ya Udhamini wa Taarifa za Juzuu la Sheria Tanzania Prof. Hamudi Majamba.

Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. George Masaju (aliyeketi katikati) akisikiliza kwa makini na kunukuu hoja za wajumbe wa Bodi ya Udhamini wa Taarifa za Juzuu la Sheria Tanzania (TLR) wakati alipotembelea na kufanya kikao na Bodi hiyo leo tarehe 21 Januari, 2026 kwenye ukumbi wa Maktaba ya Makao Makuu ya Mahakama jijini Dodoma. Kushoto ni Jaji wa Mahakama ya Rufani na Mwenyekiti wa Bodi ya Udhamini wa Taarifa za Juzuu la Sheria Tanzania (TLR), Mhe. Jacobs Mwambegele na kulia ni Katibu wa Bodi ya Udhamini wa Taarifa za Juzuu la Sheria Tanzania Prof. Hamudi Majamba.


Sehemu ya wajumbe wa Bodi wanaohudhuria kikao kazi cha Bodi ya Udhamini wa Taarifa za Juzuu la Sheria Tanzania (TLR) kinachoendelea kufanyika kwenye ukumbi wa Maktaba Makao Makuu ya Mahakama Jijini Dodoma.

Sehemu nyingine ya wajumbe wa Bodi  ya Udhamini wa Taarifa za Juzuu la Sheria Tanzania (TLR) wanaohudhuria kikao kazi kinachoendelea kufanyika kwenye ukumbi wa Maktaba Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania jijini Dodoma.

Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. George Masaju (katikati) pamoja na Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Mustapher Mohamed Siyani (wa kwanza kulia) wakisalimiana na wajumbe wa Bodi ya Udhamini wa Taarifa za Juzuu la Sheria Tanzania (TLR) mara baada ya mazungumzo na wajumbe hao yaliyofanyika kwenye ukumbi wa Maktaba Makao Makuu ya Mahakama Jijini Dodoma.

Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania Mhe. George Masaju (wa tano kulia)  akiwa katika picha ya pamoja na Wajumbe wa Bodi ya Udhamini wa Taarifa za Juzuu la Sheria Tanzania (TLR) mara baada ya mazungumzo na wajumbe hao yaliyofanyika kwenye ukumbi wa Maktaba uliopo Makao Makuu ya Mahakama Jijini Dodoma. Wa sita kulia ni Mhe. Jacobs Mwambegele, Jaji wa Mahakama ya Rufani na Mwenyekiti wa Bodi ya Udhamini wa Taarifa za Juzuu la Sheria  Tanzania (TLR) na wa kwanza kulia ni Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe.Dkt. Mustapher Mohamed Siyani.

(Picha na HABIBA MBARUKU, Mahakama-Dodoma)

 

 

 

 

 


 

 

 

 

Jumanne, 20 Januari 2026

MCHANGO WA MAHAKAMA KITUO CHA USULUHISHI KWENYE UTATUZI WA MIGOGORO HAUNA SHAKA

  • Yafanikiwa kusuluhisha mashauri yenye thamani ya zaidi ya trilioni moja
  • Jaji Mfawidhi asema usuluhishi nguzo ya ustawi, maendeleo endelevu katika Taifa

Na FAUSTINE KAPAMA-Mahakama, Dar es Salaam

Mahakama Kuu ya Tanzania, Kituo cha Usuluhishi, imefanikiwa kusuluhisha mashauri 327 yenye thamani ya Shilingi za Kitanzania 1,402,732,991,440.17 kwa mwaka 2025.

Hayo yamebainishwa na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kituo cha Usuluhishi, Mhe. Zahra Maruma, kwenye hafla ya utoaji Tuzo za Wadau wa Usuluhishi iliyofanyika jana tarehe 19 Januari, 2026 jijini Dar es Salaam.

Mhe. Maruma alibainisha kuwa mashauri hayo 327 ni kati ya 342 yaliyopokelewa kutoka Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam na Divisheni ya Ardhi katika kipindi hicho.

‘Idadi hii ilijumuisha migogoro 174 ya ardhi yenye thamani ya Shilingi za Kitanzania 161,071,243,621.51 na migogoro 153 ya madai ya kawaida yenye thamani ya Shilingi za Kitanzania 1,241,157,477,818.66,’ alisema.

Jaji Mfawidhi alibainisha pia kuwa kati ya migogoro hiyo, 47 ilihusisha Taasisi za Mabenki yenye thamani ya Shilingi za Kitanzania 148,119,498,132.26 na migogoro 56 yenye thamani ya Shilingi za Kitanzania 49,431,023,475.35 kutoka Taasisi za kiserikali.

Mhe. Maruma alisema pia kuwa katika kipindi hicho, Mahakama Kuu Kituo cha Usuluhishi ilifanikiwa kwenye upatanishi wa jumla ya mashauri 87 yenye thamani ya Shilingi za Kitanzania110,813,010,662.08 kwa makubaliano ya Shilingi za Kitanzania 36,592,613,760.31, hivyo kuokoa kiasi cha Shilingi za Kitanzania 74,220,396,901.77.

‘Kati ya mashauri hayo, kiasi cha Shilingi za Kitanzania 46,512,751,302 kiliokolewa kwa upande wa migogoro iliyohusisha Taasisi za Serikali kwa kufikia makubaliano ya Shilingi za Kitanzania 2,918,272,174 na kiasi cha Shilingi za Kitanzania 139,743,883,107 kwa migogoro ya kibenki kwa kufikia makubaliano ya Shilingi za Kitanzania 8,375,615,025,’ alisema.

Akizungumzia upande wa ngazi nyingine za Mahakama zilizosalia zikijumuisha Mahakama Kuu, Mahakama za Hakimu Mkazi na Mahakama za Wilaya, Jaji Mfawidhi alieleza kuwa jumla ya mashauri 315 yalifanikiwa kumalizika katika hatua ya usuluhishi.

Aidha, alisema kuwa Wadau wa nje ya Mahakama, kupitia Mabaraza ya Kata, Mabaraza ya Ardhi na Nyumba ya Wilaya, Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA), Maofisa Ustawi wa Jamii, Viongozi wa Dini na Wazee wa Mila, wamefanikiwa kusuluhisha migogoro 537 iliyomalizika kwa njia ya upatanishi.

‘Ukiangalia takwimi hizi utaona kupitia usuluhishi kumewezesha rasilimali hizi ambazo zilikuwa zimeshikiliwa au kuzuiliwa katika migogoro zimeweza kurudi katika mzunguko wa uchumi,’ Mhe. Maruma alisema.

Jaji Mfawidhi alieleza pia kuwa ingawa idadi ya mashauri yaliyomalizika kwa suluhu inaonekana kuwa ndogo, bado inaakisi mwelekeo chanya wa kuendelea kuimarika kwa matumizi ya usuluhishi kama nyenzo muhimu ya utatuzi wa migogoro ndani na nje ya mfumo wa Mahakama.

Alisema kuwa takwimu hizo pia si namba za kwenye karatasi, bali zinatoa tafisiri ya familia zilizookolewa dhidi ya migawanyiko na maumivu ya migogoro ambayo huwa haitibiki kwa nakala za hukumu.

Mhe. Maruma alibainisha kuwa takwimu hizo pia zinaangazia mahusiano ya kazi yaliyorejeshwa, migogoro ya ardhi iliyotamatishwa kwa amani na jamii zilizoepuka mgogoro wa kudumu.

Aidha, kupitia usuluhishi, alisema kuwa gharama nyingi zinazotokana na mgogoro huepukika, ikijumuisha rasilimali fedha na muda zinazotumika katika uendeshaji wa mashauri kupitia utaratibu wa kimahakama.

Alitaja migogoro mingine kama ushikiliaji au uzuiaji wa rasilimali zinazobishaniwa katika mgogoro kwa muda mrefu bila kuwepo katika mzunguko wa kiuchumi na ukwamishaji wa shughuli za kiuchumi kutokana na mazuio ya kisheria ambayo husababisha kudorora kwa uchumi au kuvunjika kwa mahusiano ya kibiashara au kijamii.

‘Madhara haya huweza kuepukika kwa kutatua migogoro kupitia usuluhishi. Takwimu hizi zinathibitisha kwamba usuluhishi ni nguzo ya ustawi na mshikamano na maendeleo endelevu katika Taifa letu,’ alisema Jaji Mfawidhi.

Jumla ya Tuzo 26 zilikabidhiwa kwa Wadau wa Usuluhishi mbalimbali baada ya kutambua mchango wao katika kukuza matumizi ya usuluhishi kama njia mbadala ya utatuzi wa migogoro.

Mgeni rasmi katika hafla hiyo alikuwa Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Mustapher Mohamed Siyani, aliyemwakilisha Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. George Masaju.

Waliokabidhiwa Tuzo hizo ni Majaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Naibu Wasajili, Taasisi za Umma na Serikali, Mawakili wa Kujitegemea, Halmashauri na Manispaa, Ofisi ya Ustawi wa Jamii, Tume ya Usuluhishi na Uamuzi, Taasisi za Fedha na Wasuluhishi Binafsi.


Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kituo cha Usuluhishi, Mhe. Zahra Maruma, akizungumza kwenye hafla ya utoaji Tuzo kwa Wadau wa Usuluhishi jana terehe 19 Januari, 2026 jijini Dar es Salaam.

Sehemu ya Majaji wa Mahakama Kuu na Wadau mbalimbali [juu na chini] wakiwa kwenye hafla hiyo.



Sehemu nyingine ya Majaji wa Mahakama Kuu na Wadau mbalimbali [juu na chini] wakiwa kwenye hafla hiyo.




Sehemu ya Majaji wa Mahakama Kuu na Wadau mbalimbali [juu na chini] waliokabidhiwa Tuzo kwenye hafla hiyo.



Sehemu nyingine ya Majaji wa Mahakama Kuu na Wadau mbalimbali [juu na chini] waliokabidhiwa Tuzo kwenye hafla hiyo.



Jumatatu, 19 Januari 2026

UTOAJI TUZO JUKWA MUHIMU LA KUUNGANISHA MAHAKAMA, WADAU WA USULUHISHI; JAJI MARUMA

Na HALIMA MNETE-Mahakama, Dar es Salaam

Mahakama ya Tanzania itaendeelea kutambua mchango wa wadau mbalimbali wanaoshiriki katika kuimarisha matumzi ya usuluhishi kama nyenzo muhimu ya katika utoaji wa haki, ujenzi wa amani na utulivu wa kudumu katika jamii.

Hayo yamebainishwa leo tarehe 19 Januari 2025 na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kituo cha Usuluhishi, Mhe. Zahra Maruma, kwenye hafla ya utoaji Tuzo za Wadau wa Usuluhishi kwa mwaka 2025, iliyofanyika katika Ukumbi wa Kilimanjaro, Benki Kuu ya Tanzania (BOT) jijini Dar es Salaam.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mhe. Maruma amesema tukio hilo ni jukwaa muhimu linalounganisha Mahakama na Wadau wake kwa lengo la kutafakari safari ya usuluhishi nchini, mafanikio yaliyopatikana, changamoto zilizopo pamoja na mwelekeo wa kuimarisha zaidi utamaduni wa usuluhishi kama njia mbadala na endelevu ya utatuzi wa migogoro.

Ameeleza kuwa usuluhishi si dhana mpya, bali ni sehemu ya urithi wa kitamaduni wa Watanzania uliotumika tangu enzi za mababu, na kwamba utamaduni huo umepewa msisitizo wa kikatiba chini ya Ibara ya 107A(2)(d) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, pamoja na kutambuliwa katika Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 kama nguzo ya kudumisha amani, umoja na mshikamano wa kitaifa.

Mhe. Maruma amesema utoaji wa tuzo hizo ni njia ya Mahakama kuenzi na kutambua mchango wa dhati wa Wadau wa Usuluhishi, kuhamasisha maadili, weledi na mshikamano, pamoja na kuonyesha dhamira ya Mahakama ya Tanzania katika kujenga amani ya kudumu kupitia majadiliano, mazungumzo na vikao vya suluhu vinavyoongozwa kwa hekima na busara.

Ameongeza kuwa falsafa ya usuluhishi inalenga kubadili mtazamo wa jamii kwamba haki hupatikana mahakamani pekee, akisisitiza kuwa jamvi la usuluhishi huwezesha kupata haki ya kweli kwa kurejesha mahusiano, kuondoa uhasama na kujenga maridhiano ya kudumu.

Kauli mbiu ya Tuzo za Wadau wa Usuluhishi kwa mwaka huu, Kujenga Msingi na Kuimarisha Ushiriki wa Wadau kwa Matokeo Endelevu,” ambayo ina akisi kwa kina falsafa ya usuluhishi kama mwanzo wa kurejesha amani na mahusiano, badala ya kuwa mwisho wa migogoro.

Akizungumzia ushiriki wa Wadau, Mhe. Maruma amesema mafanikio yanayoonekana yametokana na mshikamano wa Wadau mbalimbali wakiwemo Majaji, Mahakimu, Mawakili wa Serikali na wa Kujitegemea, Viongozi wa Dini na Kimila, Wasuluhishi Binafsi pamoja na Taasisi zinazotekeleza usuluhishi kwa mujibu wa sheria.

Mgeni Rasmi wa hafla hiy alikuwa Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Mustapha Mohamed Siyani, ambaye alimwakilisha Jaji Mkuu wa Mahakama ya Tanzania, Mhe. George Masaju.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mhe. Dkt. Siyani ameendelea kusisitiza kuwa usuluhishi si suala la hiari bali ni dhamira ya kikatiba, ambapo Mahakama kama chombo cha mwisho cha utoaji haki ina wajibu wa kukuza na kuendeleza mbinu za usuluhishi katika utatuzi wa migogoro.

Katika kuimarisha usuluhishi, hafla hiyo pia imeambatana na mdahalo wa kitaaluma wenye mada isemayo “Haki kwa Haraka, Mapema na Ipasavyo: Hatua za Suluhu Kabla ya Kesi,” iliyowasilishwa na Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Divisheni ya Biashara, Mhe. Abdallah Gonzi, na kujadiliwa na wabobezi wa masuala ya usuluhishi kutoka ndani na nje ya Mahakama.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kituo cha Usuluhishi, Mhe. Zahra Maruma, akizungumza kwenye hafla ya utoaji Tuzo za Wadau wa Usuluhishi. Picha chini ni Naibu Msajili wa Mahakama Mahakama Kuu Kituo cha Usuluhishi, Mhe. Augustina Mmbando.



Picha ya pamoja ya Watoa mada wakati wa hafla hiyo.


Meza Kuu inayoongozwa na Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Mustapher Mohamed Siyani [katikati waliokaa] ikiwa katika picha ya pamoja na sehemu ya Majaji Wafawidhi wa Divisheni za Mahakama Kuu.


Meza Kuu inayoongozwa na Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Mustapher Mohamed Siyani [katikati waliokaa] ikiwa katika picha ya pamoja na Majaji wa Mahakama Kuu waliohudhuria hafla hiyo.

Meza Kuu inayoongozwa na Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Mustapher Mohamed Siyani [katikati waliokaa] ikiwa katika picha ya pamoja na Wachokoza mada kwenye hafla hiyo.

Meza Kuu inayoongozwa na Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Mustapher Mohamed Siyani [katikati waliokaa] ikiwa katika picha ya pamoja na Wadau mbalimbali.


Meza Kuu inayoongozwa na Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Mustapher Mohamed Siyani [katikati waliokaa] ikiwa katika picha ya pamoja na Watumishi wa Mahakama Kuu Kituo cha Usuluhishi.

 

JAJI KIONGOZI ABAINISHA MAMBO MANNE KUIMARISHA MATUMIZI YA USULUHISHI

Na MARY GWERA, Mahakama-Dar es Salaam

Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Mustapher Mohamed Siyani amewataka Majaji, Mahakimu, Wasuluhishi, Wadau na Wananchi kwa ujumla kuzingatia na kutekeleza mambo manne muhimu ili kufikia malengo yaliyokusudiwa katika kuendeleza na kutambua umuhimu wa matumizi ya usuluhishi.

Akizungumza leo tarehe 19 Januari, 2026 katika Hafla ya Utoaji Tuzo kwa Wadau wa Usuluhishi kwa mwaka 2025 kwenye ukumbi wa Mikutano wa Benki Kuu ya Tanzania jijini Dar es Salaam, Mhe. Dkt. Siyani amesema, Mahakama imeendelea kuchukua hatua mbalimbali na kuweka vipaumbele mahususi vyenye lengo la kuhakikisha mashauri yanayosajiliwa mahakamani, yanakamilika mapema ipasavyo na usuluhishi kama sehemu ya utekelezaji wa takwa la katiba ya nchi yetu katika ibara ya 107A (2), umepewa kipaumbele kikubwa.

“Nimesikia takwimu zilizowasilishwa na Jaji Mfawidhi kuhusu mafanikio ya usuluhishi kwa mwaka 2025, ni dhahiri kwamba Mahakama na wadau wa usuluhishi wamendelea kutumia usuluhishi kama nyenzo madhubuti yenye kuaminika katika utatuzi wa migogoro. Hata hivyo, kwakuzingatia wingi wa mashauri katika nchi yetu, bado kuna nafasi zaidi kwa wananchi kutumia njia hii kutatua migogoro yao,” amesema Jaji Kiongozi.

Mhe. Dkt. Siyani ameyataja mambo manne ya kuzingatia katika kuendeleza matumizi ya Usuluhishi kuwa ni pamoja na kuongeza elimu kwa umma kuhusu usuluhishi, kuwekeza katika mafunzo endelevu, ni muhimu kuwekeza katika mafunzo ya mara kwa mara kwa wapatanishi, Matumizi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) na kuendeleza na kukuza ushirikiano wa wadau, ni kwa kupitia ushirikiano huu wa karibu kati ya Mahakama na Wadau wote.

Akizungumzia kuhusu kuongeza elimu kwa umma kuhusu usuluhishi, Jaji Kiongozi amesema, ni jukumu la Wadau wote wa Mahakama kuwaelimisha wananchi kwamba haki inaweza pia kupatikana kupitia mazungumzo, maridhiano na makubaliano yanayoheshimu maslahi ya pande zote.

Kuhusu suala la kuwekeza katika mafunzo endelevu, Mhe. Siyani ameeleza kwamba, ni muhimu kuwekeza katika mafunzo ya mara kwa mara kwa wapatanishi ili kuimarisha uelewa, mbinu za njia za usuluhishi, kutambua na kushirikiana katika kujenga mifumo yenye ufanisi na mazingira bora ya uendeshaji wa njia za usuluhishi zinazoendana na vigezo vinavyotumika katika upimaji wa mfumo wa utoaji haki wa migogoro ya madai.

Katika jambo hilo, Jaji Kiongozi amekipongeza Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto na Kituo cha Usuluhishi kwa juhudi za kuwezesha mafunzo ya njia ya upatanishi kwa Wahe Majaji na Mahakimu katika kuwajengea uwezo wa kufanya usuluhishi.

Katika matumizi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA), Mhe. Siyani amewataka Wadau wa Haki kuyazingatia kwa kuwa hayakwepeki katika zama hizi ambapo amesema, “Sote ni mashuhuda wa namna matumizi ya mifumo ya kidijitali yalivyokuwa injini ya mageuzi katika mifumo ya utoaji haki duniani. Uwekezaji katika TEHAMA si hiari, ni muhimu ili kuongeza ufanisi na upatikanaji wa huduma kwa wakati.”

Ameongeza kuwa, Mahakama kupitia mageuzi ya teknolojia, mifumo kama Mfumo wa Kielektroniki wa Usimamizi wa Mashauri (e-CMS) na Usuluhishi Mtandao(Virtual/Online Mediation) yameleta mapinduzi makubwa katika upatikanaji wa huduma za usuluhishi na kwamba matumizi ya teknolojia yamepunguza kwa kiasi kikubwa gharama, muda unaotumika kufika mahakamani, pamoja na nguvu kazi inayohitajika na hivyo kuongeza upatikanaji wa haki bila vikwazo.

Aidha, kuhusu jambo la kuendeleza na kukuza ushirikiano wa wadau, Jaji Kiongozi amesema kuwa, ushirikiano wa karibu kati ya Mahakama na Wadau wote ndio utakaohakikisha kuwa usuluhishi unakuwa njia yenye matokeo endelevu, inayotekelezeka na inayokubalika katika jamii.

Kupitia ushirikiano huu tutaweza kujenga msingi wa kujenga taifa linalothamini mazungumzo, linaloweka mbele maridhiano na linajenga mfumo wa utoaji haki unaotazama utu na maendeleo ya watu wake,” amesisitiza.

Katika hafla hiyo, Mhe. Dkt. Siyani amewajuza Wadau wote wa Mahakama kuwa kutakuwa na Wiki ya Usuluhishi na kuwaomba wadau wote wa usuluhishi na wanufaika wa huduma hizi, kuweka juhudi za pamoja katika kufanikisha wiki hiyo ambayo ni ya kihistoria na inayotarajiwa kutoa fursa nyingi za kutoa elimu ya usuluhishi.

Niwaombe pia wananchi kutumia fursa hii katika kupata elimu na kutatua migogoro kwa njia rahisi na kukuza utamaduni na desturi za kiafrika katika kutatua migogoro nje ya Mahakama kwa njia za maridhiano, hasa kwa kuzingatia uwepo wa Wapatanishi na Wasuluhishi binafsi ambao hivi sasa wanatambulika kisheria,” amesema Jaji Kiongozi.

Kadhalika, Mhe. Dkt. Siyani ametoa wito kwa wadau wote wa mfumo wa utoaji haki, kuchagua njia za usuluhishi kwa mujibu wa sheria, badala ya kupitia mchakato mrefu, wa gharama wa kimahakama unaohitaji kusubiri hukumu ambayo wakati mwingine huongeza maumivu ya mgogoro badala ya kutibu majeraha ya mgogoro kama ilivyo katika njia za usuluhushi ambazo msingi wake mkuu ni maridhiano.

Sambamba na hilo, Mhe. Dkt. Siyani pia wananchi kutumia fursa ya wiki hiyo katika kupata elimu na kutatua migogoro kwa njia rahisi na kukuza utamaduni na desturi za kiafrika katika kutatua migogoro nje ya Mahakama kwa njia za maridhiano, hasa kwa kuzingatia uwepo wa Wapatanishi na Wasuluhishi binafsi ambao hivi sasa wanatambulika kisheria.

Hafla hiyo imebeba kauli mbiu isemayo; 'Kujenga maelewano na kuimarisha ushiriki wa wadau katika upatanishi kwa matokeo endelevu.'



Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Mustapher Mohamed Siyani akizungumza leo tarehe 19 Januari, 2026 wakati wa Hafla ya Utoaji Tuzo kwa Wadau wa Usuluhishi kwa mwaka 2025 kwenye ukumbi wa Mikutano wa Benki Kuu ya Tanzania jijini Dar es Salaam.

Picha mbalimbali za Majaji, watumishi wengine wa Mahakama, Wadau  wa Mahakama wakifuatilia hotuba ya Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Mustapher Mohamed Siyani (hayupo katika picha) aliyokuwa akiitoa wakati wa Hafla ya Utoaji Tuzo kwa Wadau wa Usuluhishi leo tarehe 19 Januari, 2026 kwenye ukumbi wa Mikutano wa Benki Kuu ya Tanzania jijini Dar es Salaam.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania Kituo cha Usuluhishi, Mhe. Zahra Maruma akizungumza wakati wa Hafla ya Utoaji Tuzo kwa Wadau wa Usuluhishi kwa mwaka 2025 leo tarehe 19 Januari, 2026 kwenye ukumbi wa mikutano wa Benki Kuu ya Tanzania jijini Dar es Salaam.


Naibu Msajili wa Mahakama Kuu Kituo cha Usuluhishi, Mhe. Augustina Mmbando akizungumza 
wakati wa Hafla ya Utoaji Tuzo kwa Wadau wa Usuluhishi kwa mwaka 2025 leo tarehe 19 Januari, 2026 kwenye ukumbi wa mikutano wa Benki Kuu ya Tanzania jijini Dar es Salaam.

Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Mustapher Mohamed Siyani (katikati) wakiwa katika picha ya pamoja na Waliopokea tuzo kwenye Hafla ya Utoaji Tuzo kwa Wadau wa Usuluhishi kwa mwaka 2025 iliyofanyika leo tarehe 19 Januari, 2026 kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Benki Kuu ya Tanzania jijini Dar es Salaam.


Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Mustapher Mohamed Siyani (katikati) wakiwa katika picha ya pamoja na Watumishi wa Mahakama Kuu Kituo cha Usuluhishi kwenye Hafla ya Utoaji Tuzo kwa Wadau wa Usuluhishi kwa mwaka 2025 iliyofanyika leo tarehe 19 Januari, 2026 kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Benki Kuu ya Tanzania jijini Dar es Salaam.


Meza Kuu ikiongozwa na Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Mustapher Mohamed Siyani (katikati) wakiwa katika picha ya pamoja na Watoa Mada kwenye Hafla ya Utoaji Tuzo kwa Wadau wa Usuluhishi kwa mwaka 2025 iliyofanyika leo tarehe 19 Januari, 2026 kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Benki Kuu ya Tanzania jijini Dar es Salaam.

Meza Kuu ikiongozwa na Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Dkt. Mustapher Mohamed Siyani (katikati) wakiwa katika picha ya pamoja na Majaji walioshiriki kwenye Hafla ya Utoaji Tuzo kwa Wadau wa Usuluhishi kwa mwaka 2025 iliyofanyika leo tarehe 19 Januari, 2026 kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Benki Kuu ya Tanzania jijini Dar es Salaam.